Skip to main content

Kenya ni Kipenzi

 


Kenya ni Kipenzi

Kenya ni kipenzi, nchi tulivu
Amani kaipa Mungu, daima milele
Natujivunie wana wake, tumpongeze
Kila siku, tuwe wakushukuru.

Kenya ni Kipenzi, kweli yapendeza
Tsavo, Amboseli – mbuga za wanyama
Kericho, Limuru – chai tamu sana
Kilifi, Kisumu – fuo zenye kung’aa.

Kenya ni kipenzi, nchi tulivu
Amani kaipa Mungu, daima milele
Natujivunie wana wake, tumpongeze
Kila siku, tuwe wakushukuru.

 

Pale Turkana – chimbuko la binadamu
Bonde la ufa – muujiza wake Muumba
Mombasa sawa– kisiwa shwari raha
Historia yetu tukufu – Amu (Tamu) Lamu.

Kenya ni kipenzi, nchi tulivu
Amani kaipa Mungu, daima milele
Natujivunie wana wake, tumpongeze
Kila siku, tuwe wakushukuru.

Wakenya watu wa bidii, sio wakaidi
Ukarimu pasi kuigwa, roho ya utu
Wanariadha wake sifika, ulimwengu
Kilimo, utalii, uvumbuzi, na mengi zaidi.


Kenya ni kipenzi, nchi tulivu
Amani kaipa Mungu, daima milele
Natujivunie wana wake, tumpongeze
Kila siku, tuwe wakushukuru.

Hata katika wakati wa dhiki, Kenya kweli ni nchi barikiwa na teule. Mandhari yake ni yenye kuvutia na wananchi wake wakarimu ajabu. Ndiposa ni vyema kujiuliza, ‘Nini naweza kuifanyia nchi yangu ili iimarike zaidi?’

https://www.youtube.com/watch?v=Qq7CX3yk8r4

Comments